{"id":676,"date":"2022-07-21T09:33:19","date_gmt":"2022-07-21T09:33:19","guid":{"rendered":"https:\/\/greenagriculturetz.com\/?p=676"},"modified":"2022-07-21T09:33:19","modified_gmt":"2022-07-21T09:33:19","slug":"kilmo-bora-cha-migomba","status":"publish","type":"post","link":"https:\/\/greenagriculturetz.com\/new\/kilmo-bora-cha-migomba\/","title":{"rendered":"KILMO BORA CHA MIGOMBA"},"content":{"rendered":"\n<h2 class=\"wp-block-heading\"><\/h2>\n\n\n<div class=\"wp-block-image\">\n<figure class=\"aligncenter size-full\"><img fetchpriority=\"high\" decoding=\"async\" width=\"640\" height=\"427\" src=\"https:\/\/greenagriculturetz.com\/new\/wp-content\/uploads\/2022\/07\/DSC04598.jpeg\" alt=\"\" class=\"wp-image-677\" srcset=\"https:\/\/greenagriculturetz.com\/new\/wp-content\/uploads\/2022\/07\/DSC04598.jpeg 640w, https:\/\/greenagriculturetz.com\/new\/wp-content\/uploads\/2022\/07\/DSC04598-300x200.jpeg 300w, https:\/\/greenagriculturetz.com\/new\/wp-content\/uploads\/2022\/07\/DSC04598-633x422.jpeg 633w, https:\/\/greenagriculturetz.com\/new\/wp-content\/uploads\/2022\/07\/DSC04598-301x201.jpeg 301w, https:\/\/greenagriculturetz.com\/new\/wp-content\/uploads\/2022\/07\/DSC04598-600x400.jpeg 600w\" sizes=\"(max-width: 640px) 100vw, 640px\" \/><\/figure>\n<\/div>\n\n\n<h2 class=\"wp-block-heading\">Na Eng Octavian Lasway<\/h2>\n\n\n\n<p>Hapa Tanzania kilimo cha migomba kimekuwepo Kwa miaka mingi. Kilimo hiki ni&nbsp;maarufu sana kwa sababu zao la ndizi limekuwa likitumika kama chakula kikuu kwa&nbsp;baadhi ya mikoa kama vile Kagera, Kilimanjaro na Mbeya na hivyo kulifanya zao hili liwe la muhimu,&nbsp;kufuatia mazao ya mahindi, mpunga, mtama, muhogo,viazi na mazao ya jamii ya&nbsp;kunde kama vile maharage.<\/p>\n\n\n\n<p>Zao la ndizi linaweza kuwa moja kati ya mazao ya biashara iwapo litazalishwa kwa&nbsp;kufuata kanuni bora za uzalishaji wa zao hilo, ikwa ni pamoja na kupanda aina bora&nbsp;ya migomba inayozaa ndizi zinazotambulika katika masoko ya kimataifa.<\/p>\n\n\n\n<h2 class=\"wp-block-heading\"><br>ASILI YA MIGOMBA<\/h2>\n\n\n\n<p>Asili ya migomba ni nchi za Malaysia na India ambazo ziko Kusini Mashariki mwa&nbsp;Asia. Migomba inayolimwa sasa imetokana na migomba ijulikanayo kama&nbsp;Musa balbisiana&nbsp;ambayo asili yake ni India, na&nbsp;Musa acuminata&nbsp;ambayo asili yake ni Malaysia.<br>Kutoka Malaysia na India migomba ilifika Afrika Mashariki katika karne ya tano<\/p>\n\n\n\n<h2 class=\"wp-block-heading\"><br>MAENEO YANAYOLIMWA MIGOMBA NCHINI<\/h2>\n\n\n\n<p>Nchini Tanzania mikoa inayoshughulika na kilimo cha migomba na kuzalisha zao la&nbsp;ndizi kwa wingi ni pamoja na Kagera, Kilimanjaro, Mbeya, Arusha, Manyara, Mara,&nbsp;Tanga, Morogoro, Kigoma, na Pwani. Hata hivyo zao hili linaendelea kuenea katika<br>mkoa mingine nchini ikiwa ni pamoja na Dar es salaam,, Mwanza, Ruvuma, Shinyanga na Lindi Pia Dodoma na Singida.<br>Kilimo cha migomba kinaweza kufanyika katika kipindi chote cha mwaka kulingana na&nbsp;kiasi na mtawanyiko wa mvua hasa mabondeni au kwa umwagiliaji.<\/p>\n\n\n\n<h2 class=\"wp-block-heading\">MATUMIZI<\/h2>\n\n\n\n<h2 class=\"wp-block-heading\">Kilimo cha migomba kina faida nyingi, baadhi ya faida za migomba na&nbsp;zao la ndizi ni: &#8211;<\/h2>\n\n\n\n<p>\u2022 Zao la chakula<br>\u2022 Zao la Biashara<br>\u2022 Kutengenezea pombe(banana wine)<br>\u2022 Kulisha mifugo<br>\u2022 Kutengenezea mbolea (mboji)<br>\u2022 Matandazwa shambani (mulches)<br>\u2022 Kutoa kivuli<br>\u2022 Kutoa nyuzi<br>\u2022 Kutengenezea vitu vya sanaa<br>\u2022 Kamba<br>\u2022 Malighafi ya kutengeneza vyakula na vinywaji mbalimbali.<br>\u2022 Dawa<br>\u2022 Majani kama miamvuli, sahani, vikombe na kata<br>\u2022 Kuezekea.<\/p>\n\n\n\n<h2 class=\"wp-block-heading\">Ndizi kwa ajili ya chakula hutumika kwa kutengeneza vitu mbalimbali-:<\/h2>\n\n\n\n<p>\u2022 Makangale (Banana figs)<br>\u2022 Poda (Powder)<br>\u2022 Chenge (chips)<br>\u2022 Jeya (flakes),<br>\u2022 Juisi,<br>\u2022 Lahamu (jam)<br>\u2022 Vinywaji baridi, kama soda<br>\u2022 Mvinyo (Wine)<br>\u2022 Pombe kali<br>\u2022 Hamira<\/p>\n\n\n\n<h2 class=\"wp-block-heading\">UZALISHAJI<\/h2>\n\n\n\n<p>Zao la ndizi likizalishwa kwa utaalamu unaokubalika huweza kutoa mazao yenye&nbsp;ubora wa hali ya juu na kuongeza uzalishaji kwa eneo.&nbsp;<\/p>\n\n\n\n<h3 class=\"wp-block-heading\">Mambo yafuatayo yafaa kuzingatiwa katika uzalishaji wa zao hili.<\/h3>\n\n\n\n<h4 class=\"wp-block-heading\">(a) Hali ya hewa<\/h4>\n\n\n\n<p>Kiasi cha chini cha mvua kifaacho ni 100mm kwa mwezi au 1200mm kwa mwaka.&nbsp;Mwinuko ni kutoka usawa wa bahari hadi mita 1800 juu ya usawa wa bahari. Zaidi ya&nbsp;mwinuko huo migomba haikui vizuri. Kiasi cha joto kinachofaa ni nyuzi joto za sentigredi 25 hadi 30 chini ya nyuzi joto 16 migomba haikui vizuri.<\/p>\n\n\n\n<h4 class=\"wp-block-heading\">UDONGO<\/h4>\n\n\n\n<p>&nbsp;Migomba hustawi vizuri&nbsp;kwenye udongo wenye rutuba ya kutosha, kina kirefu, usiotuamisha maji na pia usiwe&nbsp;na chumvi. Chachu ya udongo inafaa iwe kati ya pH 5 hadi 8 kwa hiyo ni vizuri ukapima udongo ili kujua uhakika zaidi &#8230;wasiliana nasi kwa ajili ya kupima udongo(0763347985)<\/p>\n\n\n\n<h4 class=\"wp-block-heading\">(b) Aina za ndizi<\/h4>\n\n\n\n<p>Kuna aina nyigi sana za ndizi. Nchini Tanzania ndizi zinazozalishwa, zipo za aina&nbsp;nyingi ambazo hutofautiana kwa majina kutokana na eneo au mkoa unaozalisha. Hata&nbsp;hivyo zinaweza kugawanywa katika makundi mawili. Aina ambayo huliwa kwa kuzichoma, kukaanga au kupikwa zikichanganywa na vyakula vingine kama vile nyama.<br>Aina za ndizi hizo ni pamoja na Mzuzu, Mshale, Matoke, Bokoboko na Mkono wa&nbsp;Tembo.<br>Aina nyingine ni zile ambazo huliwa kama matunda, aina hizo ni kama vile Kisukari,Kimalindi, Mzungu na Mtwike.<br>Kuna aina nyingine za ndizi ambazo kwa sasa huzalishwa hapa nchini ambazo zina&nbsp;fahamika kwa ubora wake katika masoko ya ndizi ya kimataifa. Aina hizi ni pamoja na<br>Williams, Grand Naine, Pazz, Jamaica, Gold Finger, Nyingine ni Uganda green, Embwailuma Giant na Chinese Cavendish.<\/p>\n\n\n\n<h3 class=\"wp-block-heading\">(c) Utayarishaji wa shamba<\/h3>\n\n\n\n<p>Safisha sehemu inayohusika kwa kutumia zana ulizonazo.<br>Ng\u2019oa visiki vyote na mizizi yake yote&nbsp;Lima sehemu hyo kwa kutumia jembe la mkono, rato, au trekta ili kuwezesha mizizi<br>laini ya migomba kupenya ardhini kwa urahisi.<br>Baada ya visiki na magugu yote kuondolewa na hivyo ardhi kuwa wazi, uchimbaji wa&nbsp;mashimo ya kupandikiza machipukizi au miche ya migomba unaweza kufanyika.<\/p>\n\n\n\n<h4 class=\"wp-block-heading\">(d) Nafasi ya kuchimba mashimo<\/h4>\n\n\n\n<p>Mashimo yatachimbwa kwa nafasi inayokusudiwa kutumika kati ya mashina ya&nbsp;migomba na kati ya mistari kama ifuatavyo:-<br>1. Migomba inaweza kupandwa kwa nafasi ya Umbali wa meta 2.75 kwa 2.75 kwa<br>migomba mifupi kama Kimalindi na Kisukari. (Mashina 1,331 kwa hekta )<br>2. Umbali wa meta 3 kwa meta 3 kwa migomba ya urefu wa kati kama Jamaica na<br>Mshale (Mashina 1,110 kwa hekta)<br>3. Umbali wa meta 3.6 kwa meta 3.6 kwa migomba mirefu zaidi kama Uganda green<br>Mashina 760 kwa hekta).<\/p>\n\n\n\n<h4 class=\"wp-block-heading\">(e) Uchimbaji mashimo.<\/h4>\n\n\n\n<p>Uchimbaji mashimo inafaa ufanywe mapema kiasi cha juma moja hadi mwezi kabla&nbsp;ya muda wa kupanda. Shimo lichimbwe kwa kutenganisha udongo wa juu na wa chini.&nbsp;Vipimo vya shimo ni vyema vikazingatiwa. Iwapo utachimba shimo la mviringo litafaa<br>liwe na kipenyo cha sentimeta 60 hadi 90 na kina cha sentimeta 60 hadi 90. Iwapo&nbsp;utachimba shimo la mstatili au mraba litakuwa na urefu, upana na kina cha sentimeta&nbsp;60 hadi 90, kutegemea kiasi cha mbolea kilichopo na kiasi cha mvua kinachonyesha&nbsp;sehemu hiyo. Uwekaji wa mbolea hufuatia mara baada ya mashimo kuwa tayari. Kiasi&nbsp;cha debe 5 za mbolea ya samadi iliyooza vizuri au mboji iwekwe kwenye lundo la&nbsp;udongo wa juu kando ya kila shimo na ichanganywe kisha mchanganyiko wa mbolea&nbsp;na udongo urudishiwe katika shimo kisha kijiti kichomekwe katikati ya shimo hilo, ilikuonyesha sehemu ambapo mche au chipukizi litapandwa.<\/p>\n\n\n\n<h4 class=\"wp-block-heading\">(f) Kuchagua machipukizi bora<\/h4>\n\n\n\n<p>Machipukizi mazuri yanayofaa kwa mbegu ni yale yenye sifa hizi hapa chini: &#8211;<\/p>\n\n\n\n<p>Sifa za chipukizi bora<\/p>\n\n\n\n<p>Liwe chipukizi sime, yaani lenye majani membamba na siyo chipukizi maji yaani lisiwe&nbsp;lenye majani mapana.<br>Litoke kwenye mgomba (shina) wenye afya nzuri, usiokuwa na magonjwa, minyoo ya&nbsp;mizizi, wala vifukusi vya migomba.<br>Litoke kwenye mgomba wenye sifa ya kuzaa mikungu mikubwa.<br>Liwe na afya nzuri na lisiwe na dalili za ugonjwa, wadudu, au mayai ya vifukusi.<br>Urefu uwe kati ya meta 1 na meta 2<br>Kipenyo cha sehemu ya chini ya shina la chipukizi (tunguu) kiwe ni kati ya sentimeta<br>15 hadi 25.<\/p>\n\n\n\n<h4 class=\"wp-block-heading\">(g) Upandaji wa machipukizi<\/h4>\n\n\n\n<p>Wakati unaofaa kupanda machipukizi ni mwanzoni mwa msimu wa mvua. Chomoa&nbsp;kile kijiti na chimba shimo la kiasi cha sentimeta 30&#215;30 katikati ya shimo lililojazwa&nbsp;mchanganyiko wa udongo na samadi kisha panda chipukizi hilo.<br>Rudishia udongo na hakikisha tunguu lote limefunikwa vizuri. Shindilia udongo ili&nbsp;chipukizi lisimame wima imara. Machipukizi yanayo tarajiwa kupandwa yanatakiwa&nbsp;kuondolewa mizizi yote ili kudhibiti minyoofundo na fukuzi wa migomba. Pia maji ya<br>moto au dawa kama vile furadani inaweza kutumika kuulia wadudu kwenye mizizi ya&nbsp;migomba.<\/p>\n\n\n\n<h2 class=\"wp-block-heading\">UTUNZAJI WA SHAMBA NA MIMEA.<\/h2>\n\n\n\n<h4 class=\"wp-block-heading\">(a) Uwekaji wa matandazwa (mulching)<\/h4>\n\n\n\n<p>Kazi hii ni vyema ikafanywa mara baada ya kupanda kama inawezekana. Matandazo&nbsp;yawe ni makavu na unene wa sentimeta 15 ili kuhifadhi unyevu, kuzuia magugu na&nbsp;yakioza yataongeza mbolea.<\/p>\n\n\n\n<h4 class=\"wp-block-heading\">(b) Uongezaji wa mbolea<\/h4>\n\n\n\n<p>Baada kupanda ni vyema kuongeza mbolea madebe 2 kuzunguuka shina la migomba&nbsp;kila baada ya miaka miwili au mitatu. Mbolea hii inatakiwa kuchanganywa na udongo&nbsp;na kufunikwa kwa matandazwa.<\/p>\n\n\n\n<h4 class=\"wp-block-heading\">(c) Umwagiliaji maji shambani<\/h4>\n\n\n\n<p>Migomba huhitaji maji mengi. Wakati wa kiangazi. Inafaa kumwagilia ili kuto kupunguza sana ukubwa na wingi wa ndizi zinazotarajiwa kuvunwa kwa mwaka. Kiasi cha maji&nbsp;kinachotakiwa kwa wiki ni milimita 25, yaani eneo linalo zunguka shina la migomba&nbsp;lilowe kabisa.<\/p>\n\n\n\n<h4 class=\"wp-block-heading\">(d) Kupunguzia machipukizi<\/h4>\n\n\n\n<p>Inatakiwa kupunguza mimea ya migomba kwa kila shina na kubaki mimea mitatu tu,&nbsp;yaani Mgomba wenye ndizi (Mama), Mgomba mkubwa ambao bado haujazaa lakini&nbsp;unakaribia kuchanua (Mtoto), Mgomba mchanga uliochipua hivi karibuni ( Mjukuu)<\/p>\n\n\n\n<h4 class=\"wp-block-heading\">(e) Uondoaji wa Majani Makavu<\/h4>\n\n\n\n<p>Mimea ya migomba inafaa iondolewe majani yote makavu ili kuondoa uwezekano wa&nbsp;kuwepo mazalia ya wadudu na magonjwa, kuruhusu mionzi ya jua na kufanya urahisi&nbsp;wa kuhudumia shamba .Pia hufanya shamba kuonekana safi.<\/p>\n\n\n\n<h4 class=\"wp-block-heading\">(f) Uondoaji wa ncha mwishoni mwa matunda<\/h4>\n\n\n\n<p>Baada ya mkungu kutoa ndizi, ua hunyauka na kubakiza ncha mwishoni mwa matunda. Ncha hizo hupaswa kuondolewa .Huduma hii husaidia kupunguza uwezekano wa<br>kujeruhi matunda wakati wa kusafirisha jambo ambalo kupunguza ubora wa tunda.<\/p>\n\n\n\n<h4 class=\"wp-block-heading\">(g) Kuweka Miega<\/h4>\n\n\n\n<p>Miega ni nguzo au kamba ambazo hutumika kuzuia migomba iliyobeba mikungu mikubwa isianguke kutokana na uzito mkubwa na upepo. Miega ni ya lazima katika sehemu zenye&nbsp;upepo mkali. Kazi hii inatakiwa kufanywa kwa uangalifu ili isijeruhi ndizi na mgomba&nbsp;wenyewe.<\/p>\n\n\n\n<h4 class=\"wp-block-heading\">(h) Uondoaji wa kichombezo cha ua la kiume (Shumba)<\/h4>\n\n\n\n<p>Uondoaji wa shumba huwezesha matunda kukua vizuri, kuongezeka uzito wa mkungu&nbsp;pia huzuia magonjwa kama vile ugonjwa wa mnyauko wa migomba (Banana Baterial<br>Wilt), ugonjwa wa Majivu nchani mwa matunda (Cigar end rot). Ukataji hufanyika juu&nbsp;ya kovu la pili baada ya kichana cha mwisho, kwa kutumia kisu kikali.<\/p>\n\n\n\n<h2 class=\"wp-block-heading\">UVUNAJI WA NDIZI<\/h2>\n\n\n\n<p>Zao la ndizi huweza kuanza kuvunwa katika kipindi cha miezi 9 hadi miezi 15 tangu&nbsp;kupandwa kwa chipukizi. Muda wa kuvunwa hutegemea hali ya hewa. Katika sehemu&nbsp;za joto ndizi huvunwa mapema zaidi kuliko sehemu za baridi. Pia migomba iliyopandwa kwa kutumia machipukizi huzaa mapema kuliko iliyopandwa miche iliyozalishwa&nbsp;kwa chupa (tissue culture)<\/p>\n\n\n\n<h2 class=\"wp-block-heading\">MATUMIZI YA RIBONI<\/h2>\n\n\n\n<p>Riboni za rangi moja (au alama ya kamba) hufungwa kwenye migomba ya umri mmoja mara tu inapoanza kuchanua, na riboni ya rangi nyingine hufungwa kwenye migomba itakayoanza kuchanua wiki mbili hivi zinazofuata na kuendelea hivyo ili kurahisisha<br>kuitambulisha mikungu ambayo itavunwa kwa wakati mmoja. Pia matumizi ya riboni&nbsp;hurahisisha utunzaji wa kumbukumbu ili kujua ni lini na ni mikungu mingapi itavunwa.<\/p>\n\n\n\n<h2 class=\"wp-block-heading\">WAKATI UNAOFAA KUVUNA<\/h2>\n\n\n\n<p>Mkungu wa ndizi huweza kuvunwa katika hatua tofauti kulingana na matumizi, aina&nbsp;na mahitaji ya soko. Mkungu huachwa kwenye mgomba mpaka vidole (matunda )&nbsp;vimejaa. Uzito wa mkungu hongezeka haraka katika wiki mbili za mwisho, ambapo&nbsp;migongo ya ndizi hutoweka.&nbsp;Ndizi zinaweza kuvunwa zikiwa zimekomaa na zimeiva kwa kiasi cha asilimia 75 kwa&nbsp;ajili ya kusafirishwa mbali, pia zinaweza kuvunwa zikiwa zimekomaa na zimeanza kuiva&nbsp;kwa ajili ya soko la karibu, au zikiwa zimekomaa na kuiva kabisa kwa ajili ya soko na&nbsp;matumizi ya nyumbani Njia bora ya kukata mkungu, ni ile inayohakikisha kuwa mkungu wa ndizi hauanguki chini na kuvunjika, kuchubuana au kuharibu ndizi, jambo ambalo<br>litapunguza ubora. Ukichelewa kuvuna ndizi zinaweza kuharibiwa na ndege, wanyama, wadudu au kuibiwa.<\/p>\n\n\n\n<h2 class=\"wp-block-heading\">UBORA WA NDIZI<\/h2>\n\n\n\n<p>Ndizi zenye sifa nzuri sokoni ni zile ambazo zimekomaa kwa kiasi kinachotakiwa na&nbsp;zenye vidole vyenye urefu mzuri na visivyo na michubuko. Pia ziwe hazijashambuliwa&nbsp;na magonjwa wala wadudu waharibifu.<\/p>\n\n\n\n<h2 class=\"wp-block-heading\">KIASI CHA MAVUNO<\/h2>\n\n\n\n<p>Mavuno ya ndizi hutegemea zaidi aina ya migomba, hali ya hewa, utunzaji wa mimea&nbsp;shambani. Mavuno huweza kufikia hadi tani 60 au zaidi kwa hekta kwa mwaka. Hata&nbsp;hivyo mavuno mazuri kwa mkulima wa kawaida yasipungue kati ya tani 20 hadi 30&nbsp;kwa hekta kwa mwaka.<\/p>\n\n\n\n<h2 class=\"wp-block-heading\">MAGONJWA<\/h2>\n\n\n\n<p>Ugonjwa wa hatari sana ulioingia hivi karibuni katika wilaya ya Muleba na maeneo&nbsp;mengine mkoani Kagera kutoka nchi jirani ya Uganda ni wa&nbsp;Mnyauko wa migomba<br>unaosababishwa na bakteria (Banana Bacterial Wilt). Magonjwa mengine yanayosumbua zao hili ni Kuoza tunguu, Ugonjwa wa panama, Ugonjwa wa majivu nchani mwa<br>tunda, Sigatoka, na Moko.<\/p>\n\n\n\n<h2 class=\"wp-block-heading\">WADUDU WAHARIBIFU<\/h2>\n\n\n\n<p>Wadudu wanaosumbua zaidi hili ni Minyoo fundo (Banana nematodes), na Vifukuzi<br>(Banana weevils).<\/p>\n\n\n\n<h2 class=\"wp-block-heading\">UDHIBITI WA MAGONJWA NA WADUDU WAHARIBIFU<\/h2>\n\n\n\n<p>Magonjwa na wadudu hawa huweza kuepukwa kwa kufuata kanuni bora za uzalishaji&nbsp;wa zao hili. kama usafi wa shamba na kuchagua chipukizi bora. Au kupanda miche&nbsp;iliyozalishwa kwa chupa (Tissue culture banana seedlings) Hata hivyo mara mataizo&nbsp;haya yakitokea muone mtaalamu wa kilimo aliye karibu ili aweze kukupa ushauri wa&nbsp;dalili za ugonjwa wa mnyauko wa migomba unaosababishwa na bakteria Mbolea inayofaa wakati wa upandaji ni samadi kama vile kinyesi cha ng\u2019ombe.<\/p>\n\n\n\n<p class=\"has-text-align-center\">Octavian Lasway<br>Irrigation and water resources engineer<br>076334985<\/p>\n","protected":false},"excerpt":{"rendered":"<p>Na Eng Octavian Lasway Hapa Tanzania kilimo cha migomba kimekuwepo Kwa miaka mingi. Kilimo hiki ni&nbsp;maarufu sana kwa sababu zao la ndizi limekuwa likitumika kama chakula kikuu kwa&nbsp;baadhi ya mikoa kama vile Kagera, Kilimanjaro na Mbeya na hivyo kulifanya zao hili liwe la muhimu,&nbsp;kufuatia mazao ya mahindi, mpunga, mtama, muhogo,viazi na mazao ya jamii ya&nbsp;kunde&#8230;<\/p>\n","protected":false},"author":1,"featured_media":677,"comment_status":"open","ping_status":"open","sticky":false,"template":"","format":"standard","meta":{"footnotes":""},"categories":[49],"tags":[],"class_list":["post-676","post","type-post","status-publish","format-standard","has-post-thumbnail","hentry","category-agronomy","item-inner"],"_links":{"self":[{"href":"https:\/\/greenagriculturetz.com\/new\/wp-json\/wp\/v2\/posts\/676","targetHints":{"allow":["GET"]}}],"collection":[{"href":"https:\/\/greenagriculturetz.com\/new\/wp-json\/wp\/v2\/posts"}],"about":[{"href":"https:\/\/greenagriculturetz.com\/new\/wp-json\/wp\/v2\/types\/post"}],"author":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/greenagriculturetz.com\/new\/wp-json\/wp\/v2\/users\/1"}],"replies":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/greenagriculturetz.com\/new\/wp-json\/wp\/v2\/comments?post=676"}],"version-history":[{"count":0,"href":"https:\/\/greenagriculturetz.com\/new\/wp-json\/wp\/v2\/posts\/676\/revisions"}],"wp:featuredmedia":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/greenagriculturetz.com\/new\/wp-json\/wp\/v2\/media\/677"}],"wp:attachment":[{"href":"https:\/\/greenagriculturetz.com\/new\/wp-json\/wp\/v2\/media?parent=676"}],"wp:term":[{"taxonomy":"category","embeddable":true,"href":"https:\/\/greenagriculturetz.com\/new\/wp-json\/wp\/v2\/categories?post=676"},{"taxonomy":"post_tag","embeddable":true,"href":"https:\/\/greenagriculturetz.com\/new\/wp-json\/wp\/v2\/tags?post=676"}],"curies":[{"name":"wp","href":"https:\/\/api.w.org\/{rel}","templated":true}]}}